Header Ads


WATU 24 WAGUNDULIKA KUUGUA UGONJWA WA KIPINDU PINDU MKOANI MBEYA HUKU WAWILI WAKIFARIKI DUNIA KUTOKANA NA UGONJWA HUO








Mbeya
WATU 24 wamegundulika kuugua ugonjwa wa kipindupindu huku mmoja akifariki dunia wilayani Kyela mkoani Mbeya na kuzuka hofu kubwa kwa viongozi wa serikali ngazi ya wilaya  ambao wamekutana pamoja na wadau wengine kutafuta namna ya kuutokomeza ugonjwa huo hatari.
Akitoa taarifa mbele ya kikao cha kamati ya afya iliyokutana jana kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo,mganga mkuu wilayani humo,Dkt,Mariam Gwere Alisema uliibuka tarehe 17/11/2017 ambapo wagonjwa wawili walipelekwa zahanati ya Dream care iliyopo Njisi wagonjwa hao kutoka kijiji cha mbako kata ya Ikimba.
Amesema baada ya wagonjwa hao kuchukuliwa vipimo,walibainika kuwa wanamaambukizi ya ugonjwa huo wa kipindupindu na siku iliyofuata walibainika wengine kutoka maeneo mbalimbali.
Ameongeza kuwa kutokana na hali hiyo maafisa afya na wakuu wengine wa idara wametawanyika maeneo mbalimbali hasa kata zilizo pembezoni mwa mto kiwira ambao ni chanzo kikuu cha mlipuko huo baada ya wagonjwa wa awali kuonekana kutumia maji ya mto huo yaliwa hayajachemshwa wala kuwekwa dawa.
Alisema mpango mkakati waliouanza ni kuhakikisha visima vyote vinawekwa dawa za kutubu maji,na kutoa eleimu kwa umma juu ya kuchemsha maji ya kunywa,kunawa mikono na sabuni pindi watokapo chooni na kujenga vyoo bora na safi.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo,Mussa Mgatta,alisema kwa sasa wametenga maeneo matatu ambayo yatatumika kwa ajili ya kuwahifadhi na kuwatibu wagonjwa watakaobainika kuambukizwa ugonjwa huo.

No comments

Powered by Blogger.