BMT YATANGAZA KAMATI ITAKAYO SIMAMIA MCHEZO WA NGUMI ZA KULIPWA
Katibu
mkuu wa baraza la michezo la taifa BMT Mohamed Kiganja ametangaza kamati maalum
itakayosimamia mchezo wa ngumi za kulipwa ikiwa ni ahadi iliyotolewa na waziri
wa habari, sanaa, utamaduni na michezo Harrison Mwakyembe wakati akipokea
rasimu ya katiba Februari 03.
Kiganja
ametangaza majina ya kamati hiyo hukua kieleza kwa kina namna itakavyokua
ikifanya kazi kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa.
Wakati huo huo Kiganja amewataka wadau wa michezo nchini kufuata utaratibu wa kuwasilisha malalamiko yao kwa lengo la kutatua migogoro inayoibuka kwa pande mbili ambazo huibuka mara kwa mara.



Post a Comment