AMRI YA KAMANDA WA JESHI LA POLISI MKOANI SONGWE YA WARUDISHA MADEREVA BARABARANI
MBOZI-SONGWE
Na manuel kaminyoge
Baadhi ya madereva hao christofa mwakyusa na fredy
kamali wakiongea na kituo hiki mwishoni mwa wiki wamesema wameamua kugoma kwa
kushinikiza wenzao waliokamatwa ili waachiwe na kuongeza kuwa wamekuwa
wakikamatwa na maaskari hao na kutozwa faini bila risti kitu ambacho kinawapa
wasiwasi kuhusu faini hizo .
Daimondi kinyampanda amesema kuwa hawapo tayari kupeleka gari zao
barabarani mpaka wenzao waliokamatwa waachiwe na kuongeza kuwa wapo tayari
kukaa muda wowote bila kupeleka magari barabarani.
Mmoja wa wamiliki wa
magari hayo maka mahenge amesema kuwa wao kama wamiliki wa magari hayo
hawautambui mgomo huo na kumuumba kamanda nyange awape kibali watafute madaleva
wengine ili yaendelee kutoa huduma ya usafiri.
afisa mfawidhi sumatra mkoa wa songwe Faith ntukamazina amesema kuwa
waliotayari kufanya kazi wafanye na watakao kaidi watachukuliwa sheria kali na
kuongeza kuwa wao kama Sumatra hawana taarifa za mgomo huo.
Kwa upande wake kamanada
wa jeshi la polisi mkoa wa songwe matiusi
nyange amesema kuwa yeyote aliyetayari
kupeleka gari barabarani apeleke na asiye taka afutiwe reseni yake kwani mgomo
wa madreva hao haujafuata taratibu na sheria .
mwishoo.
contact :0762306521 /mwabhulye93@gmail.com


Post a Comment