URUSI YAANZA VIZURI KOMBE LA MABARA
URUSI
Urusi mwenyeji wa kombe la mabara imeanza vizuri jana baada ya kuishinda New Zealand kwa mabao 2-0.
Timu zote zilisimama uwanjani wakisikiliza hotuba iliyotolewa na rais wa Urusi Vladimir Putin na rais wa shirikisho na kandanda duniani Gianini Infantino , kabla ya kuruhusiwa kukamilisha maandalizi ya pambano hilo.
Siku chache kabla , Putin aliwataka wachezaji wa timu hiyo kupata matokeo mazuri ili kuweza kuwafurahisha wananchi wa Urusi.
Leo ni kati ya Ureno mabingwa wa bara la Ulaya dhidi ya Mexico.

Post a Comment